Skip to main content

BARUA KWA WILLIAM RUTO by Mohammed Ali

Hujambo bwana kusema na kutenda. Naomba safari hii kabla hujatenda nikujulishe mawili hivi. Najua huna raha, hupati usingizi na unahofia maisha yako licha ya utajiri uliyonayo. Leo hii umejipata kubanwa na uliowaamini. Ndoa za haraka na tama zina shida bwana Ruto. Ukipenda viazi usiogope mimba ndio msemo wetu kule vilima vya raha. Ndoa yako na Uhuru Kenyatta imefikia kiwango cha mtu mmoja kati yenu kupata mimba. Si mimba ya mtoto bali mimba ya machungu na kusalitiana. Miaka ya nyuma kabla ya wewe kuwa HUSTLER wa kizazi kipya niliwahi


kukutembelea mara kwa mara katika afisi zako katika jumba la Transnational. Tulizungumza na kutaniana na hata kuzungumza kwa simu. Ulikuwa machachari na mtu wa watu. Mwaka wa 2007/ 2008 baada ya ghasia za baada ya uchaguzi wewe na Raila mlikuwa chanda na pete mkijaribu kuunda serikali ya muungano na kupigania nafasi ya ukubwa wa wana odm katika serikali hiyo iliyowaibia kura. Katika pilka pilka hizo usaliti wa hali ya juu ulitendeka.

Wabakaji wa demokrasia walianza kunoa kisu huku nyinyi mkidhani mambo yalikuwa yashakwisha. Baada ya kufanyiwa unyama na PNU nilidhani mmejifunza mawili kuhusiana na ndoa za kipumbavu. Lakini naona mlisahau kuwa
ukila na kipofu kuwa mwangalifu kwani akikosa nyama atakushika mkono. Sasa nahofia chakula cha jubilee kimeisha na vipofu wote wanataka kukushika wewe mkono uwe kitoweo chao cha mwisho. Hamna anayekupenda, wewe ulikuwa chombo, chombo cha kuwavukisha wao kutoka masaibu yao. Kila mwenda kwa mganga lazima atoe kafara na kafara ni wewe. Nahofia utafungwa ama utakuwa mkimbizi wa ndani kwa ndani na ndio hio siku utajua masaibu ya kuishi kama wakimbizi wa ndani kwa ndani mwaka wa 2007/8. Utakuwa huna raha, utadhalilishwa, utakuwa mnyonge bila haki na hatimaye utakuwa huna maana kwa serikali ya TNA. Wacha niseme TNA kwa sababu URP haina usemi tena. URP imebakwa peupe wazi wazi, URP inalea mimba haramu, mimba ya kujitakia.


William Ruto usidanganywe na maombi za kinafiki zinazotekelezwa na wafuasi na maadui wako. Kama unataka kutatua shida zako binafsi na maombi tasa pole. Maombi ni ya kuondoa usinzi, wanaofumaniwa na wake za watu, mapepo na kumshukuru mungu na kumwogopa. Sio safari za mahakamani. Ruto, imefika wakati wa kucheza karata yako ya mwisho. Katika kucheza kwako jiepushe na Adan Duale na Kipchumba Murkomen hawa wawili ni wajuzi wa ligi za kitoto au wacha niseme ligi za mchezo wa tufe( mpira wa karatasi) unaochezwa na watoto. Hawatokusaidia ila watazidi kuongeza kuni kwenye moto. Moses Kuria anafanya yanayofanywa na Duale na Kipchumba ndani ya TNA sasa moto umewaka na ni sharti chakula kipikwe.

Kabla wakupike janjaruka. Kenya imekuwa taifa la kuzalisha wanafiki na watu waoga. Tumekubali ukiritimba itawale. Profesa hana tofauti na mtoto wa darasa la kwanza. Jiepushe na wanaokuzunguka na kujifanya wasomi ila ni watu wa maslahi. Maji tayari yamemwagika lakini ni wewe kuamua mkondo wa maji hayo. Huna budi kurudi kwa marafiki zako wa zamani kwani tayari wakenya washajua kikulacho ki nguoni mwako. Kwa maoni yangu binafsi na naomba unikosoe ni wewe kujiondoa mara moja kwenye muungano wa kinafiki. Warudie uliowakosea na uombe msamaha hakika Mungu anatuamrisha kuwasamehe maadui. Najua ni aibu kwako lakini kumbuka una familia. Aidha usiwahi kuwaona ama uishi bila ya kuwaona. Uamuzi umo mikononi mwako. Kuna uwezekano wa kujifunza na haya na kuamua kuunda muungano wa ukombozi wa tatu kina nyinyi mkiwa nyuma muwaachie vijana usukani. Kuna ile kadi moja ya mwisho ya wewe kuwatumia wana URP kupasisha mswaada na wana CORD wa kumwondoa Uhuru Kenyatta mamlakani kwa wingi wa kura bungeni lakini kwa yale umewafanyia wakenya miaka mitatu sioni kama CORD itakubali uwe Rais kwa miaka miwili iliyosalia kwa mujibu wa katiba ya Kenya. Bwana Ruto huu ni wakati wako wakuwaza na kuwazua. Tunazo changamatoto zinazotukabili kama taifa. Badala ya kukaa na kujiuliza kwa nini tuko hapa na tutatoka vipi, tunakaa na kuongea mambo ya kinafiki na ukabila. Akili ndogo kutawala akili kubwa. Watu wenye akili kubwa wanaweka akili zao mfukoni kwa sababu ya ushabiki wa kivyama badala ya kukaa na kutatua matatizo ya wakenya. Bunge limekuwa bunge la kitototo. Wakenya sasa wanataka bunge la mapinduzi. Badala ya kuwazomea wakenya waskilizeni.


Deni la Kenya linazidi kuongezeka. Kila mkenya anadaiwa hata mimba inadaiwa. Ndio taifa tuliyonayo sasa. Williama Samoei Arap Ruto huna la ziada sasa. Tayari chama chako na uongozi wako umebakwa ki-demokrasia. Waswahili wanasema mimba ya mwanaharamu huingia mara moja ya pili ni kusudi. Je, ulisahau mimba ya mwaka wa 2007? Kwa nini umekubali mimba nyengine mwaka wa 2013? Umechezewa shere tangu na mwanzo wa ndoa yenu ya vichochoroni. Huna sura sasa, wakenya hawatokukubali tangu watoto wao wapigwe na vitoa machozi wakipigania uwanja wa shule yao ya msingi wa langata. Huna sura tena, ufisadi umekuwa jina lako la pili. Wakenya hawakuamini tena. Iwapo ulijikakamua na kuwasaidia wakenya tangu mchukue uongozi leo hii wangekusitiri na kukupokea lakini ulisahau kuna kupanda na kushuka. Leo zamu ya kushuka kukutana na sisi kina yahe. Hatutakudhulumu wala kukuita majina, sisi tutaoongozwa na dini na hekima.

Karibu nyumbani lakini kumbuka sisi hatuna nguvu za kukusaidia maana sote ni maskini kama mlivyotufanyia mlipokuwa masimba. Mlitufanya maskini kwa kutudhulumu na uongozi wenu wa kusema na kuenda. Leo bwana Ruto hakuendeki. Huna budi kumkumbatia Raila Amollo Odinga na kumwomba msamaha kwa semi zako za chuki dhidi yake. Akufaye kwa dhiki ndiye rafiki. Kumbuke hata simba ni mkali lakini hutiwa mimba. Kuwa na ijumaa njema. Ni mimi rafiki wako wa zamani, Mohammed Ali.
Mohammed Ali ni Mhariri Mkuu wa Kitengo cha Upekuzi KTN.

Kuwasiliana naye:

mali@standardmedia.co.ke,

FB: Official Jicho Pevu with Mohammed Ali,

Twitter: @mohajichopevu


TWAOMBA RADHI.
Katika makala ya wiki iliyopita ( kuna serikali kweli Kenya ), tulisema kuwa tangu jubilee iingie mamlakani, wakenya zaidi ya laki tatu wamepoteza maisha yao kutokana na hali mbaya ya usalama. Tungelipenda kusahihisha na kusema kuwa tulikuwa tukimaanisha watu zaidi ya 300.




>>>>..link >>> https://www.facebook.com/Official.JichoPevu/posts/1050381778346741


Comments

Popular posts from this blog

11 Habits You Need to Stop Doing

Stop watching too much TV If you spend too much time watching TV, you are wasting your life away. I feel really strongly about this one. I don’t have cable, and while I do watch some shows on Netflix, it’s few and far between. I only watch TV after I really am relaxed and need a break. I’m also careful not to turn on the TV right when I get home. I find that if I do this, I’m sucked in. This is why I keep my reading list and focus on reading good books instead. So, start to pay attention to how much TV you’re watching. If you think it’s too much, cut back. Limit your TV intake to 30 minutes to 1 hour per day, if possible. Stop talking about people behind their backs Talking about someone behind her back is a bad idea for a number of reasons. First, if someone is talking to you behind someone else’s back, you can bet on it that they also will talk about you. Second, did you know that when you talk about someone negatively, the person who you’re talking to will associate yo

John Deere Tractor for sale Asking price 850,000/-

The details are as follows: Make - John Deere (Original from Germany) Reg No: KTCB271G Model - 3130 Configuration: 2WD 97hp Color- Green & Yellow YOM: 1980 Fuel: Diesel Asking 850,000/- Asking price 850,000/- It has brand new front tyres and 70%(new) rear tyres. It is a very powerful Machine and it is an original John Deere in serviceable and working condition. The tractor can serve you in different fields like ploughing and transportation of things like sugarcane etc For more picture kindly check below If interested please give me a call on +254726687369 (Davis) The Tractor is currently stationed in Chemelil,Kisumu County

Boss Discovered My Side Job And Threatened To Fire Me!!

Here is Judy’s Story I have been working for my current boss for close to 3 years now. The job is okay, it’s just that my salary has not been increased during this whole time. I have been struggling to make ends meet and to be honest, I have been surviving on loans from here and there. A few months back, a friend of mine introduced me to a guy who offered me an online job and a salary that is equal to the one that my boss pays me. The job was so flexible, so I quickly agreed to do it. To juggle the two jobs, I have been getting to work very early and then I start with the workload for my ‘actual’ job and then when I am done, I tackle the other job which is so much more flexible and easier. I have really been enjoying this because every end of the month, I get not one, but two pay checks. I have found financial freedom that I never thought was possible. I can even afford to save cash for the future However, I am afraid I messed up and it may cost me my job. I got to work very